Andes
From Wikipedia, the free encyclopedia
Andes ni safu ya milima kunjamano na safu ndefu kabisa ya milima duniani. Inaendana na urefu wote wa Amerika Kusini upande wa magharibi wa bara hili, ikiongozana na mstari wa pwani ya Pasifiki kutoka Kolombia katika kaskazini hadi Chile katika kusini. Urefu wa safu yote ni takriban km 7,500. Milima ya juu inafikia kimo cha m 6,962 na wastani wa milima yote uko kwenye m 4000. Upana wa milima hii ni kati ya km 200 na 600.