Mtindo wa Kigothi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtindo wa Kigothi (pia: Gotiki, kwa Kiingereza: Gothic style, Gothic architecture) katika usanifu majengo wa Ulaya ni mtindo ulioanza katika karne ya 12 na kutumika hadi mnamo 1500. Mtindo huo ulichukua nafasi ya mtindo wa Kiroma uliotumika kabla yake. Ulionekana pia katika matawi mengine ya sanaa. Katika karne ya 19 ulitumika upya kwa majengo makubwa katika mtindo wa Kigothi mamboleo.