Ugonjwa wa moyo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ugonjwa wa moyo ni maradhi yanayoushambulia na kuudhoofisha moyo. Moyo ni kiungo kinachosukuma damu katika mwili wa kiumbe hai, hasa wanyama. Damu hiyo huwa na vitu kama oksijeni, homoni, seli za damu na virutubishi mbalimbali kutoka katika vyakula anavyokula. Ugonjwa wa moyo mara nyingi huwapata binadamu kuliko wanyama wengine.