Bantustan
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bantustan ilikuwa jina la eneo maalumu katika Afrika Kusini wakati wa siasa ya Apartheid (ubaguzi wa rangi wa kisheria). Eneo hilo lilitenganishwa kwa ajili ya kabila fulani la Waafrika asili. Kimsingi ilikuwa kama rizavu katika makoloni ya Uingereza, lakini chini ya siasa ya Apartheid ilitangazwa kuwa nchi ya pekee.