Donald "Flash" Gordon
From Wikipedia, the free encyclopedia
Donald "Flash" Gordon (17 Julai 1920 - 4 Januari 2010) alikuwa rubani shujaa wa vita wa Marekani. Alipiga risasi zaidi ya ndege 7 za Ujapani katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Alikuwa rubani wa kivita wa Kikosi cha Wanamaji wa Marekani na alipokea tuzo ya Distinguished Flying Cross.