Western
From Wikipedia, the free encyclopedia
Western (kutoka kiing. "West" - magharibi) ni aina ya fasihi, hadithi na filamu yenye asili katika Marekani. Western husimulia hadithi za watu walioishi wakati wa karne ya 19 hadi mwanzo wa karne ya 20 Marekani ilipoenea katika sehemu za magharibi ya Amerika ya Kaskazini. Filamu kuhusu kipindi hiki zilianza kupatikana tangu mwanzo wa karne ya 20.
Kazi muhimu ya hadithi hizo ilikuwa kuwapa watu wa Marekani picha kuhusu historia yao na kuhusu tabia nzuri ya mababu walioanzisha na kueneza taifa lao. Ukweli wa kihistoria jinsi ilivyo katika hadithi za kitaifa haukuzingatiwa mara nyingi.
Filamu za Western zilitengenezwa baadaye pia huko Ulaya hasa Spaghetti Western na mara nyingi zilicheza na aina za wahusika jinsi zilivyokuwa kawaida katika filamu za Marekani.