Peloponesi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Peloponesi (Kigiriki Πελοπόννησος peloponesos) ni rasi ya kusini mwa Ugiriki. Imeunganika na sehemu ya bara ya nchi kwa shingo la nchi kwenye mji wa Korintho.
Jina la kihistoria la rasi lilikuwa Morea (Μωριάς morias).
Eneo lote la Peloponesi ni kilomita za mraba 21,549. Kuna watu 1,155,000 walioishi huko mwaka 2011.
Peninsula imegawanywa kati ya mikoa mitatu ya kiutawala: sehemu kubwa ni ya mkoa wa Peloponesi, na sehemu ndogo ni za mkoa wa Ugiriki Magharibi na wa Attica.