Soya
From Wikipedia, the free encyclopedia
Soya ni aina ya maharagwe na mbegu za msoya (Glycine max) katika familia Fabaceae. Asili yake iko Asia ya Mashariki.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Soya (Glycine max) | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Soya | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
|
Funga
Ni zao la mafuta na sifa yake ya pekee ni kiasi kikubwa cha protini katika mbegu zake (40-50%). Kutokana na lishe yake kubwa kilimo chake kimeenea duniani. Kwa watu wasiokula nyama, mafuta ya soya na vyakula vinavyotokana na soya yana mahitaji yote ya protini kwa gharama ndogo.
Rangi ya mbegu zake huwa ni njano, nyeupe lakini kuna pia aina za kahawia.