Spika (muziki)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Spika ya muziki (kutoka Kiingereza: Loudspeaker) ni chombo kinachobadilisha kawi za audio zilizo katika mfumo wa elektroniki na kuzifanya ziwe sauti.
Spika zinazotumika siku hizi zilivumbuliwa na Edward Kellog na Chester Rice mwaka 1925.
Spika hufanya kazi kama kipazasauti. Tofauti ni kuwa kipazasauti hubadilisha sauti kuwa audio zilizo kwa mfumo wa kielektroniki ilhali spika nazo hubadilisha kawi hii kuwa sauti.
Kwa kawaida, spika huwekwa katika chumba au kabineti ambayo mara nyingi huwa na umbo la mstatili au mraba. Kabineti ya spika huenda ikatengenezwa kwa plastiki au mbao. Hili huathiri jinsi sauti itakavyokuwa.