Antibiotiki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Antibiotiki (kutoka Kiingereza antibiotics, mara nyingine Kiuavijasumu[1]) ni kemikali ambazo hutumika kuua au kuzuia ukuaji wa bakteria zinazosababisha magonjwa.
Mwanzo neno antibi otiki lilitumika kuelezea kemikali zinazotengenezwa na bakteria au kuvu, ambazo ni sumu kwa viumbehai wengine. Kwa sasa neno linatumika kujumuisha kampaundi ogania (kemikali za kaboni zinazopatikana katika viumbehai) zinazotengenezwa na zile zinazopatikana kwa kuchanganya asilia na bandia.
Antibiotiki nyingi huwa ni sumu kwa bakteria; hata hivyo, kwa kuwa neno limekuwa likitumika pia kuelezea madawa ambayo hutumika kuzuia magonjwa kama malaria, na yale yanayosabibishwa na virusi au protozoa. Antibiotiki zote zina tabia ya kuwa na uchaguzi inapotumika kama sumu. Zinakuwa hatari sana kwa viumbe vinavyoingia ndani ya kiumbe kingine kuliko vile vinavyokuwa ndani ya mnyama au binadamu ambaye hutumia kama tiba.
Penicillin ni miongoni mwa antibiotiki zinazofahamika sana na imekuwa ikitumika kupambana na magonjwa mengi ya kuambukiza kama vile kaswende, kisonono na pepopunda. Antibiotiki nyingine, streptomycin imekuwa inatumika kupambana na kifua kikuu.