Barbara Cui Lianzhi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Barbara Cui Lianzhi (Xiaotian, 1849 hivi - Liushuitao 15 Juni 1900) alikuwa mwanamke wa China aliyefia imani ya Ukristo wakati wa Uasi wa Mabondia. Baada ya kuuliwa mwanae alijaribu kukimbia usiku lakini akakamatwa na kuteswa vikali hadi kifodini chake[1].
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu pamoja na wengine 119 tarehe 1 Oktoba 2000.
Sikukuu yao ya pamoja huadhimishwa tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe ni tarehe 15 Juni, siku ya kifodini chake[2].