Filipo Neri
From Wikipedia, the free encyclopedia
Filipo Neri (Firenze 22 Julai 1515 - Roma 27 Mei 1595), alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mwanzilishi wa shirika la Waoratori.
Ni maarufu kama "mtume wa Roma" kutokana na kazi yake bora aliyoifanya katika mji huo katika karne ya 16. Akijitahidi kuepusha vijana na dhambi, alianzisha oratori, vilipofanyika masomo ya kiroho, nyimbo na matendo ya huruma. Aling'aa kwa upendo wake kwa jirani, kwa unyofu wa Kiinjili, kwa furaha ya kudumu, kwa bidii ya pekee na kwa ari katika kumtumikia Mungu[1].
Alitangazwa na Papa Paulo V kuwa mwenye heri tarehe 11 Mei 1615, halafu tarehe 12 Machi 1622 Papa Gregori XV alimtangaza mtakatifu.