Fransisko Ferdinando de Capillas
From Wikipedia, the free encyclopedia
Fransisko Fernández (au Ferdinando) de Capillas, O.P. (15 Agosti 1607 – 15 Januari 1648) alikuwa padri kutoka Hispania aliyefanya umisionari Ufilipino na barani Asia akafungwa muda mrefu akauawa kwa kukatwa kichwa huko Fu’an, nchini China kwa ajili ya imani yake ya Kikristo wakati wa dhuluma ya Watartari.[1]
Alitangazwa kuwa mtakatifu pamoja na wengine 119 waliofuata kifodini chake na Papa Yohane Paulo II tarehe 1 Oktoba 2000.[2]
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake, lakini pamoja na wenzake ni tarehe 9 Julai[3].