Somo la Kimungu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Somo la Kimungu (kwa Kilatini: Lectio Divina), hasa somo la Biblia, ni kati ya njia kuu za utakatifu zilizotolewa kwa Wakristo wote[1]. Mara nyingi udanganyifu, uzushi na uhuni vinaambukiza kupitia vitabu vibaya, kumbe “kusoma vitabu vitakatifu ni uzima wa roho” (Ambrosi).