Bata-shimo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mabata-shimo ni ndege wa maji wa nusufamilia ya Tadorninae katika familia ya Anatidae. Mabata hawa ni katikati ya mabata wachovya na mabata bukini kwa ukubwa na kwa umbo. Wanaitwa mabata-shimo kwa sababu spishi nyingi hutaga mayai ndani ya shimo la mti au pango la sungura, mhanga n.k. Hula wanyamakombe, kaa, wadudu, nyungunyungu au manyasi, mimea ingine na mbegu. Wakiruka angani wanafanana zaidi na mabata bukini kuliko na mabata wachovya.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Bata-shimo | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Bata bukini wa Misri | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 10:
| ||||||||||||
Funga