Fransisko wa Asizi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Fransisko wa Asizi (kwa Kiitalia Francesco d'Assisi; tangu utotoni jina la ubatizo Giovanni (Battista), yaani Yohane, liliachwa kutumika; pia ubini mwana wa Petro Bernardone ulikuja kuachwa baada ya wao kushindana) alikuwa mtawa, shemasi na mhubiri wa Kanisa Katoliki.
Alizaliwa mwaka 1181 au 1182 mjini Assisi, Italia; alifariki tarehe 3 Oktoba 1226 karibu na mji ule.
Anakumbukwa kwa mtindo wa maisha alipolenga kuiga mfano wa Yesu kila siku.
Alianzisha jumuiya ya kitawa yenye matawi mbalimbali ambayo leo ni utawa wenye wafuasi wengi kuliko yote wakikadiriwa kukaribia milioni moja duniani kote.
Kwa Wakatoliki ni msimamizi wa wanaoshughulikia hifadhi ya mazingira.
Alitangazwa na Papa Gregori IX kuwa mtakatifu tarehe 16 Julai 1228.
Anaheshimiwa na wengi hata nje ya Kanisa lake.