Funguvisiwa la Karolini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Funguvisiwa la Karolini (kwa Kiingereza: Caroline Islands) ni funguvisiwa la Mikronesia lililosambaa sana katika Bahari ya Pasifiki hadi umbali wa kilomita 3,540[1]. Ni visiwa vidogo 500 hivi vyenye asili ya matumbawe.
Sehemu kubwa ni ya Shirikisho la Mikronesia, ila Palau ni nchi huru ya pekee.