Kitabu cha Mormoni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kitabu cha Mormoni ni mwandiko wa kidini wa jumuiya ya Wamormoni walioitwa hivyo kufuatana na jina la kitabu hicho. Wenyewe huamini ni kitabu kitakatifu chenye neno la Mungu.
Mormoni anatajwa kama nabii na kiongozi wa kidini anayetambulishwa mle kama mhariri wa kitabu. Kitabu cha Mormoni kilitolewa mwaka 1830 na Mmarekani Joseph Smith, Mdogo aliyedai kuwa alitafsiri kitabu kutoka kwa mabamba ya dhahabu aliyopewa na malaika wa Mungu.