Kipululu
From Wikipedia, the free encyclopedia
-Kwa kiunzi cha binadamu tazama makala "Kiunzi cha mifupa"-
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kipululu | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kipululu wa Afrika (Turnix sylvaticus lepurana) | ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
Jenasi 2, spishi 17:
| ||||||||||
Funga
Vipululu (pia vipururu) ni ndege wa familia Turnicidae. Spishi moja inaitwa kiunzi pia (tazama orodha ya spishi). Ndege hawa wanafanana tombo lakini hawana mnasaba na hawa. Wana rangi ya mchanga na madoa meusi au kahawia. Hawapendi kupuruka. Jike ana rangi kali kuliko dume na huanzisha ubembelezi. Dume huatamia na hutunza makinda.
Ndege hawa waliainishwa zamani ndani ya Gruiformes (oda ya makorongo) au Galliformes (oda ya kuku). Lakini utafiti wa ADN umeonyesha kama vipululu wana mnasaba na vitwitwi. Kwa hivyo wanaainishwa ndani ya Charadriiformes sasa. Kisukuku kimefunuliwa ambacho kimetambuliwa kama jamaa wa vipululu na kuitwa Turnipax.