Kwenzi au kuzi ni ndege wadogo kiasi wa familia Sturnidae. Spishi nyingine zinaitwa kizole au nyangala. Wanatokea Ulaya, Afrika, Asia na Australia. Baadhi ya spishi zimewasilishwa katika Amerika ya Kaskazini, Nyuzilandi na Afrika. Wanapenda kuwa kwa makundi. Spishi nyingi zina rangi ya buluu, pengine pamoja na rangi kali kama nyekundu, machungwa na njano; spishi nyingine ni nyeusi, kijivu au kahawia, pengine pamoja na nyeupe, njano, nyekundu au pinki. Sauti yao ina utata na huiga sauti za mazingira, kama ndege wengine, kamsa za magari na hata msemo wa binadamu. Ndege hawa hula wadudu na matunda hasa, lakini hula nusra kila kitu. Takriban spishi zote hulijenga tago lao katika tundu. Jike huyataga mayai 2-6 meupe au buluu.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kwenzi |
Kwenzi maridadi |
Uainishaji wa kisayansi |
Himaya: |
Animalia (Wanyama)
|
Faila: |
Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
|
Ngeli: |
Aves (Ndege)
|
Oda: |
Passeriformes (Ndege kama shomoro)
|
Familia ya juu: |
Muscicapoidea (Ndege kama shore)
|
Familia: |
Sturnidae (Ndege walio na mnasaba na kwenzi) Rafinesque, 1815 |
Spishi: |
Angalia katiba
|
|
Ngazi za chini |
Jenasi 33:
- Acridotheres Vieillot, 1816
- Agropsar Oates, 1889
- Ampeliceps Blyth, 1842
- Aplonis Gould, 1836
- Basilornis Bonaparte, 1850
- Cinnyricinclus Lesson, 1840
- Creatophora Lesson, 1847
- Enodes Temminck, 1839
- Fregilupus Lesson, 1831
- Gracula Linnaeus, 1758
- Gracupica Lesson, 1831
- Grafisia Bates, 1926
- Hartlaubius Bonaparte, 1853
- Hylopsar Boetticher, 1941
- Lamprotornis Temminck, 1820
- Leucopsar Stresemann, 1912
- Mino Lesson, 1827
- Necropsar Slater, 1879
- Neocichla Sharpe, 1876
- Notopholia Roberts, 1922
- Onychognathus Hartlaub, 1849
- Pastor Temminck, 1815
- Poeoptera Bonaparte, 1854
- Rhabdornis Reichenbach, 1853
- Sarcops Walden, 1875
- Saroglossa Hodgson, 1844
- Scissirostrum Lafresnaye, 1845
- Speculipastor Reichenow, 1879
- Spodiopsar Sharpe, 1889
- Streptocitta Bonaparte, 1850
- Sturnia Lesson, 1837
- Sturnornis Legge, 1879
- Sturnus Linnaeus, 1758
|
Funga