London
Mji mkuu wa Uingereza na wa Ufalme wa Muungano / From Wikipedia, the free encyclopedia
London ni mji mkuu wa Uingereza na mji mkubwa wa nchi hii wenye wakazi milioni 7.5. Kwenye rundiko la mji idadi ya watu ni karibu milioni 14.
- Tazama pia East London, Afrika Kusini; London, Ontario na New London, Connecticut
Ukweli wa haraka Nchi, - Wakazi kwa ujumla ...
London | |
Mahali pa mji wa London katika Uingereza |
|
Majiranukta: 51°30′28″N 00°07′41″W | |
Nchi | Ufalme wa Muungano |
---|---|
Idadi ya wakazi (2007) | |
- Wakazi kwa ujumla | 7,556,900 |
Tovuti: http://www.london.gov.uk/ |
Funga
London ni mahali muhimu kwa biashara na benki kimataifa. Jiji la London ndilo linalopokea watalii wengi zaidi ulimwenguni.[1] Uwanja wa ndege wa Heathrow unapokea wasafiri wengi zaidi kushinda mahali popote duniani.[2]
London ina watu wa kutoka tamaduni mbalimbali, dini tofautitofauti, na zaidi ya lugha 300 huzungumzwa jijini London.[3]
Mji umepambwa na majengo mazuri kama makumbusho, makanisa na majumba yanayovuta watalii wengi kila mwaka.