Mkopo (fedha)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mkopo (kutoka kitenzi "kukopa"; kwa Kiingereza: "loan") wa kifedha ni pesa ambazo mtu au shirika anapewa na benki, asasi ya fedha ya ushirika (SACCOS)[1], kundi au mashirika mengine yaliyoidhinishwa kufanya biashara ya fedha. Anayepata mkopo huwa na deni analofaa kulipa kulingana na makubaliano rasmi yake na anayemkopesha. Deni hili linaweza kuwa karadha[2] au mkopo unaolipwa pamoja na riba[3]. Riba ndiyo faida ya mashirika kama benki yanayofanya biashara ya ukopeshaji.