Pembetatu ya Kionga
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pembetatu ya Kionga ilikuwa eneo dogo la kilomita za mraba 395 [1] kwenye Bahari ya Hindi, kusini kwa Mto Rovuma na kaskazini mwa Rasi Delgado. Ndani ya eneo hilo kuna mji wa Kionga (kwa Kireno "Quionga"), ambao mwaka wa 1910 ulikuwa na wakazi karibu 4,000.
Eneo hilo lilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini tangu mwaka 1918 ni sehemu ya Msumbiji.