Teresa wa Mtoto Yesu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Teresa wa Mtoto Yesu na wa Uso Mtakatifu, O.C.D. (Alençon, Ufaransa, 2 Januari 1873 - Lisieux, Ufaransa, 30 Septemba 1897) ni jina la kitawa la Thérèse Françoise Marie Martin, maarufu pia kama Teresa wa Lisieux, anayeheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu mwenye sifa za bikira na mwalimu wa Kanisa.
Akifurahia udogo wake, Teresa alijitokeza kama “mtaalamu wa elimu ya upendo” (Papa Yohane Paulo II), katika maandishi yake, hasa katika shajara alimosimulia kwa unyofu wa hali ya juu jinsi kwa neema alivyoelewa na kutekeleza Injili katika maisha yake yaliyofichika ndani ya monasteri ya Wakarmeli Peku.
Tangu mwaka 1927 ni msimamizi wa wamisionari wote (pamoja na Fransisko Saveri), na tangu mwaka 1944 wa Ufaransa (pamoja na Yoana wa Arc).