Vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Marekani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Marekani ilipigwa kuanzia mwaka 1861 hadi 1865 kati ya majimbo ya kusini na majimbo ya kaskazini nchini Marekani. Mwaka 1861 kundi la majimbo ya kusini lilijitenga na Muungano wa Madola ya Amerika likajiita "Shirikisho la madola ya Amerika" (Confederate States of America). Serikali ya Muungano haikukubali hatua hiyo ukaiona kama uasi. Mashambulio ya jeshi la kusini dhidi ya vituo vya kijeshi ndani ya kusini vilivyokuwa chini ya amri ya Muungano yalianzisha vita iliyodumu hadi 1865 na kuleta ushindi wa kaskazini, yaani jeshi la Muungano. Shirikisho likavunjwa na majimbo yake kurudishwa katika Muungano. Vita hii ilileta vifo vingi, pamoja na mwisho wa utumwa katika Marekani.