Modesti Andlauer
From Wikipedia, the free encyclopedia
Modesti Andlauer, S.J. (Rosheim, 22 Mei 1847 - Wuyi 19 Juni 1900) alikuwa padri Mjesuiti kutoka Ufaransa aliyefia Ukristo akifanya umisionari nchini China wakati wa Uasi wa Mabondia.
Aliuawa pamoja na Remi Isore wakiwa wanasali mbele ya altare[1]
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu pamoja na wengine 119 tarehe 1 Oktoba 2000.
Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe tarehe 19 Juni[2].