Remi Isore
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remi Isore, S.J. (Bambecque, 22 Januari 1852 - Wuyi 19 Juni 1900) alikuwa padri Mjesuiti kutoka Ufaransa aliyefia Ukristo akifanya umisionari nchini China wakati wa Uasi wa Waboksa.
Aliuawa pamoja na Modesti Andlauer wakiwa wanasali mbele ya altare[1].
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu pamoja na wengine 119 tarehe 1 Oktoba 2000.
Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe tarehe 19 Juni[2].