Drogo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Drogo (pia: Dreux, Drugo, Druron; Epinoy, Artois, leo nchini Ufaransa, 14 Machi 1105 - Sebourg, Ufaransa Kaskazini, 16 Aprili 1186 hivi) alikuwa Mkristo aliyetamani maisha manyofu na upweke. Kwa ajili hiyo kwa miaka mingi alifanya kazi ya kuchunga na hakuwa na makao maalumu, akitembelea patakatifu mbalimbali, halafu akawa mkaapweke katika chumba kidogo kilichounganika na kanisa[1][2][3].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.