Kolumbani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kolumbani abati (Columbán, maana yake "Njiwa mweupe"; 540 - 23 Novemba 615) alikuwa mmonaki mmisionari kutoka Ireland, maarufu kwa kuanzisha monasteri nyingi na kueneza Ukristo wa Kiselti katika nchi mbalimbali za Ulaya bara, ukiwa pamoja na kanuni kali ya kitawa, malipizi, na maungamo ya binafsi kwa padri.
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, hasa siku ya kifo chake, tarehe 23 Novemba[1].