Mitume wa Yesu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtume wa Yesu Kristo (kwa Kigiriki ἀπόστολος, apóstolos, aliyetumwa), kadiri ya Agano Jipya, ni mmojawapo kati ya wale wanaume 12 ambao Yesu aliwateua mapema akawatuma kuhubiri Ufalme wa Mungu kwanza kwa taifa la Israeli, halafu kwa mataifa yote duniani.
Mitume wa Yesu |
---|
|
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Baada ya kifo na ufufuko wake, hao wakawa viongozi wa Kanisa ambalo hadi leo linajitambua kujengwa juu yao.
Habari zao, lakini hasa za Petro, zilianza kuandikwa na Mwinjili Luka katika kitabu cha Matendo ya Mitume, ambamo baadaye mhusika mkuu ni Mtume Paulo aliyedai kuteuliwa na Yesu Kristo baada ya kufufuka.