Oliver Plunkett
From Wikipedia, the free encyclopedia
Oliver Plunkett (kwa Kieire: Oilibhéar Pluincéid; Loughcrew, County Meath, Ireland, 1 Novemba 1625[1] – Tyburn, London, Uingereza, 1 Julai 1681) alikuwa askofu mkuu wa Armagh, kaskazini mwa Ireland, kuanzia mwaka 1670[2].
Baada ya njama ya Kipapa aliendelea, ingawa kwa siri, kutokana na dhuluma ya serikali.
Hatimaye alikamatwa na kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa kueneza imani Katoliki[3]. Hivyo alinyongwa na kuraruliwa akisamehe wote na kukiri imani sahihi hadi mwisho.
Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri tarehe 23 Mei 1920, halafu Papa Paulo VI tarehe 12 Oktoba 1975 alimtangaza kuwa mtakatifu mfiadini.