Simba S.C.
Timu ya mpira wa miguu / From Wikipedia, the free encyclopedia
Simba Sports Club ni timu ya soka iliyo na makao makuu katika mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, katika jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo ilianzishwa mwaka 1936, ikiitwa kwanza Eagles na baadaye tena iliitwa Dar Sunderland. Mwaka 1971 ikaibadilisha jina lake kabisa na kuitwa, Simba Sport Club (ambalo linamaanisha Lion kwa Kiinɡereza).
Simba Sports Club ni mojawapo ya timu kubwa ya mpira wa miguu nchini Tanzania, wapinzani wao wanaitwa Younɡ Africans.
Ni mabingwa wa taifa mara 18 tena ni mabingwa mara 6 katika kombe la Kagame.[1]
Mechi zao za nyumbani zinachezwa kwenye viwanja viwili, Uwanja wa Uhuru na Uwanja wa Taifa.